Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 3:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Wengi wanasema juu yangu,“Hatapata msaada kwa Mungu.”

3. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu u ngao yangu kila upande;kwako napata fahari na ushindi wangu.

4. Nakulilia kwa sauti, ee Mungu,nawe wanisikiliza kutoka mlima wako mtakatifu.

5. Nalala na kupata usingizi,naamka tena maana wewe ee Mwenyezi-Mungu wanitegemeza.

6. Sitayaogopa maelfu ya watu,wanaonizingira kila upande.

7. Uje ee Mwenyezi-Mungu!Niokoe ee Mungu wangu!Wewe wawavunja mataya maadui zangu wote;wawavunja meno waovu wasinidhuru.

8. Mwenyezi-Mungu ndiwe uokoaye;uwape baraka watu wako.

Kusoma sura kamili Zaburi 3