1. Ee Mwenyezi-Mungu, tazama walivyo wengi adui zangu,ni wengi mno hao wanaonishambulia.
2. Wengi wanasema juu yangu,“Hatapata msaada kwa Mungu.”
3. Lakini wewe ee Mwenyezi-Mungu u ngao yangu kila upande;kwako napata fahari na ushindi wangu.
4. Nakulilia kwa sauti, ee Mungu,nawe wanisikiliza kutoka mlima wako mtakatifu.
5. Nalala na kupata usingizi,naamka tena maana wewe ee Mwenyezi-Mungu wanitegemeza.