4. Uwaadhibu kadiri ya matendo yao,kufuatana na maovu waliyotenda.Waadhibu kadiri ya matendo yao wenyewe;uwatendee yale wanayostahili.
5. Hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu;hawatambui mambo aliyoyafanya.Kwa sababu hiyo atawabomoa,wala hatawajenga tena upya.
6. Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,maana amesikiliza ombi langu.
7. Mwenyezi-Mungu ndiye nguvu yangu na ngao yangu;tegemeo la moyo wangu limo kwake.Amenisaidia nami nikashangilia kwa moyo;kwa wimbo wangu ninamshukuru.
8. Mwenyezi-Mungu ni nguvu ya watu wake;yeye ni kimbilio la wokovu kwa mfalme wake mteule.
9. Ee Mungu, uwaokoe watu wako;uwabariki watu hao walio mali yako.Uwe mchungaji wao na kuwategemeza milele.