1. Ee Mwenyezi-Mungu, unitetee,maana nimeishi bila hatia,nimekutumainia wewe bila kusita.
2. Unijaribu, ee Mwenyezi-Mungu, na kunipima;uchunguze moyo wangu na akili zangu.
3. Fadhili zako ziko mbele ya macho yangu,ninaishi kutokana na uaminifu wako.
4. Sijumuiki na watu wapotovu;sishirikiani na watu wanafiki.
5. Nachukia mikutano ya wabaya;wala sitajumuika na waovu.
6. Nanawa mikono yangu kuonesha sina hatia,na kuizunguka madhabahu yako, ee Mwenyezi-Mungu,
7. nikiimba wimbo wa shukrani,na kusimulia matendo yako yote ya ajabu.