1. Mfalme ashangilia, ee Mwenyezi-Mungu, kwa nguvu yako,anafurahi mno kwa msaada uliompa.
2. Umemtimizia matakwa ya moyo wake;wala hukumkatalia ombi lake.
3. Umemjia, ukampa baraka nzurinzuri;umemvika taji ya dhahabu safi kichwani mwake.
4. Alikuomba maisha nawe ukampa;ulimpa maisha marefu milele na milele.
5. Kwa msaada wako ametukuka sana;wewe umemjalia fahari na heshima.
6. Wamjalia baraka zako daima;wamfurahisha kwa kuwako kwako.