Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 19:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Yanifunza mimi mtumishi wako;kuyafuata kwaniletea tuzo kubwa.

12. Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe?Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua.

13. Unikinge mimi mtumishi wako na makosa ya makusudi,usikubali hayo yanitawale.Hapo nitakuwa mkamilifu,wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa.

14. Maneno ya kinywa changu, na mawazo ya moyo wangu,yakubalike mbele yako, ee Mwenyezi-Mungu,mwamba wangu na mkombozi wangu!

Kusoma sura kamili Zaburi 19