1. Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu;anga ladhihirisha kazi ya mikono yake.
2. Mchana waupasha habari mchana ufuatao,usiku waufahamisha usiku ufuatao.
3. Hamna msemo au maneno yanayotumika;wala hakuna sauti inayosikika;
4. hata hivyo, sauti yao yaenea duniani kote,na maneno yao yafika kingo za ulimwengu.Mungu ameliwekea jua makao yake angani;
5. nalo hutoka kama bwana arusi chumbani mwake,lafurahi kama shujaa aliye tayari kushindana.
6. Lachomoza toka upande mmoja,na kuzunguka hadi upande mwingine;hakuna kiwezacho kuliepa joto lake.
7. Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu,humpa mtu uhai mpya;masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti,huwapa hekima wasio na makuu.
8. Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa,huufurahisha moyo;amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi,humwelimisha mtu.