Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 19:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu;anga ladhihirisha kazi ya mikono yake.

2. Mchana waupasha habari mchana ufuatao,usiku waufahamisha usiku ufuatao.

3. Hamna msemo au maneno yanayotumika;wala hakuna sauti inayosikika;

4. hata hivyo, sauti yao yaenea duniani kote,na maneno yao yafika kingo za ulimwengu.Mungu ameliwekea jua makao yake angani;

5. nalo hutoka kama bwana arusi chumbani mwake,lafurahi kama shujaa aliye tayari kushindana.

6. Lachomoza toka upande mmoja,na kuzunguka hadi upande mwingine;hakuna kiwezacho kuliepa joto lake.

7. Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu,humpa mtu uhai mpya;masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti,huwapa hekima wasio na makuu.

8. Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa,huufurahisha moyo;amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi,humwelimisha mtu.

9. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni jambo jema,na la kudumu milele;maagizo ya Mwenyezi-Mungu ni sawa,yote ni ya haki kabisa.

10. Yatamanika kuliko dhahabu;kuliko dhahabu safi kabisa.Ni matamu kuliko asali;kuliko asali safi kabisa.

11. Yanifunza mimi mtumishi wako;kuyafuata kwaniletea tuzo kubwa.

12. Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe?Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua.

Kusoma sura kamili Zaburi 19