Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 18:43-50 Biblia Habari Njema (BHN)

43. Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,ukanifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

44. Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.

45. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.

46. Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wa usalama wangu;atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.

47. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.

48. Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,akanikuza juu ya wapinzani wangu,na kunisalimisha mbali na watu wakatili.

49. Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.

50. Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.

Kusoma sura kamili Zaburi 18