37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.
38. Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.
39. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.
40. Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.
41. Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.
42. Niliwatwanga wakawa kama vumbi inayopeperushwa na upepo;niliwakanyaga kama tope la njiani.
43. Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,ukanifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.
44. Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.
45. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.