Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 18:34-50 Biblia Habari Njema (BHN)

34. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.

35. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;mkono wako wa kulia umenitegemeza;wema wako umenifanikisha.

36. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.

37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.

38. Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.

39. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.

40. Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.

41. Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.

42. Niliwatwanga wakawa kama vumbi inayopeperushwa na upepo;niliwakanyaga kama tope la njiani.

43. Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,ukanifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.

44. Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.

45. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.

46. Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wa usalama wangu;atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.

47. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.

48. Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,akanikuza juu ya wapinzani wangu,na kunisalimisha mbali na watu wakatili.

49. Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.

50. Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.

Kusoma sura kamili Zaburi 18