34. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.
35. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;mkono wako wa kulia umenitegemeza;wema wako umenifanikisha.
36. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.
37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.
38. Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.
39. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.
40. Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.
41. Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.
42. Niliwatwanga wakawa kama vumbi inayopeperushwa na upepo;niliwakanyaga kama tope la njiani.
43. Wewe uliniokoa na mashambulizi ya watu,ukanifanya mtawala wa mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.
44. Mara waliposikia habari zangu walinitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.
45. Wageni walikufa moyo;wakaja kutoka ngome zao wakitetemeka.
46. Mwenyezi-Mungu yu hai!Asifiwe mwamba wa usalama wangu;atukuzwe Mungu wa wokovu wangu.
47. Yeye ameniwezesha kulipiza kisasi;na kuyashinda mataifa chini yangu.
48. Ameniokoa kutoka kwa maadui zangu,akanikuza juu ya wapinzani wangu,na kunisalimisha mbali na watu wakatili.
49. Kwa hiyo nitakutukuza kati ya mataifa,ee Mwenyezi-Mungu nitaliimbia sifa jina lako.
50. Mungu humjalia mfalme wake ushindi mkubwa;humwonesha fadhili zake huyo mteule wake,naam, humfadhili Daudi na wazawa wake milele.