33. Ameiimarisha miguu yangu kama ya paa,na kuniweka salama juu ya vilele.
34. Hunifunza kupigana vita,mikono yangu iweze kuvuta upinde wa shaba.
35. Umenipa ngao yako ya kuniokoa;mkono wako wa kulia umenitegemeza;wema wako umenifanikisha.
36. Umenirahisishia njia yangu;wala miguu yangu haikuteleza.
37. Niliwafuatia adui zangu na kuwakamata;sikurudi nyuma mpaka nimewaangamiza.
38. Niliwaangusha chini wasiweze kuinuka tena;walianguka chini ya miguu yangu.
39. Wewe ulinijalia nguvu ya kupigana vita;uliwaporomosha maadui chini yangu.
40. Uliwafanya maadui zangu wakimbie,na wale walionichukia niliwaangamiza.
41. Walipiga yowe lakini hapakuwa na wa kuwaokoa;walimlilia Mwenyezi-Mungu lakini hakuwajibu.