21. Maana nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.
22. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.
23. Mbele yake sikuwa na hatia;nimejikinga nisiwe na hatia.
24. Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu;yeye ajua kwamba mikono yangu haina hatia.
25. Wewe ni mwaminifu kwa walio waaminifu;mwema kwa wale walio wema.
26. Wewe ni mkamilifu kwa walio wakamilifu;lakini mkatili kwa watu walio waovu.
27. Wewe wawaokoa walio wanyenyekevu,lakini wenye majivuno huwaporomosha.
28. Wewe ee Mwenyezi-Mungu, waniangazia;walifukuza giza langu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.
29. Kwa msaada wako nakishambulia kikosi;wewe wanipa nguvu ya kuruka ukuta.
30. Huyu Mungu matendo yake hayana dosari!Ahadi ya Mwenyezi-Mungu ni ya kuaminika;yeye ni ngao kwa wote wanaomkimbilia usalama.
31. Nani aliye Mungu isipokuwa Mwenyezi-Mungu?Nani aliye mwamba wa usalama ila Mungu wetu?
32. Mungu ndiye anijaliaye nguvu kila upande;ndiye anayeifanya salama njia yangu.