Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 18:13-24 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni;Mungu Mkuu akatoa sauti yake,kukatokea mvua ya mawe na makaa ya moto.

14. Aliwapiga maadui mishale yake, akawatawanya,alirusha umeme, akawatimua.

15. Ulipowakemea maadui zako ee Mwenyezi-Mungu,ulipowatisha kwa ghadhabu yako,vilindi vya bahari vilifunuliwa,misingi ya dunia ikaonekana.

16. Mungu alinyosha mkono kutoka juu akanichukua,kutoka katika maji mengi alininyanyua.

17. Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu nyingi,aliniokoa kutoka kwa hao walionichukia,maana walikuwa na nguvu kunishinda.

18. Walinivamia nilipokuwa taabuni,lakini Mwenyezi-Mungu alikuwa kinga yangu.

19. Alinileta, akaniweka mahali pa usalama;alinisalimisha, kwani alipendezwa nami.

20. Mwenyezi-Mungu alinipa tuzo kadiri ya uadilifu wangu;alinituza kwa vile mikono yangu haina hatia.

21. Maana nimefuata njia za Mwenyezi-Mungu,wala sikujitenga na Mungu wangu kwa uovu.

22. Nimeshika maagizo yake yote,sikuacha kufuata masharti yake.

23. Mbele yake sikuwa na hatia;nimejikinga nisiwe na hatia.

24. Mwenyezi-Mungu amenituza kadiri ya uadilifu wangu;yeye ajua kwamba mikono yangu haina hatia.

Kusoma sura kamili Zaburi 18