Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 18:1-16 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Nakupenda, ee Mwenyezi-Mungu, nguvu yangu!

2. Mwenyezi-Mungu ni mwamba wangu,ngome yangu na mkombozi wangu;Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia usalama;ngao yangu, nguvu za wokovu wangu na ngome yangu.

3. Namwita Mwenyezi-Mungu astahiliye sifa anisaidie,nami naokolewa kutoka kwa maadui zangu.

4. Kamba za kifo zilinizingira,mawimbi ya maangamizi yalinivamia;

5. kamba za kuzimu zilinizinga,mitego ya kifo ilinikabili.

6. Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,nilimlilia Mungu wangu anisaidie.Aliisikia sauti yangu hekaluni mwake;kilio changu kilimfikia masikioni mwake.

7. Hapo dunia ikatetemeka na kutikisika;misingi ya milima ikayumbayumba,kwani Mungu alikuwa amekasirika.

8. Moshi ulifuka kutoka puani mwake,moto uunguzao ukatoka kinywani mwake;makaa ya moto yalilipuka kutoka kwake.

9. Aliinamisha anga, akashuka chini;na wingu jeusi chini ya miguu yake.

10. Alipanda kiumbe chenye mabawa akaruka;akapaa kasi juu ya mabawa ya upepo.

11. Alijifunika giza pande zote,mawingu mazito yaliyojaa maji yalimzunguka.

12. Umeme ulimulika mbele yake;kukatokea mawinguni mvua ya mawe na makaa ya moto.

13. Mwenyezi-Mungu alinguruma kutoka mbinguni;Mungu Mkuu akatoa sauti yake,kukatokea mvua ya mawe na makaa ya moto.

14. Aliwapiga maadui mishale yake, akawatawanya,alirusha umeme, akawatimua.

15. Ulipowakemea maadui zako ee Mwenyezi-Mungu,ulipowatisha kwa ghadhabu yako,vilindi vya bahari vilifunuliwa,misingi ya dunia ikaonekana.

16. Mungu alinyosha mkono kutoka juu akanichukua,kutoka katika maji mengi alininyanyua.

Kusoma sura kamili Zaburi 18