4. Kuhusu matendo watendayo watu;mimi nimeitii amri yako,nimeepa njia ya wadhalimu.
5. Nimefuata daima njia yako;wala sijateleza kamwe.
6. Nakuita, ee Mungu, kwani wewe wanijibu;unitegee sikio, uyasikie maneno yangu.
7. Onesha fadhili zako za ajabu,uwaokoe kutoka kwa adui zao,wale wanaokimbilia usalama kwako.
8. Unilinde kama mboni ya jicho;unifiche kivulini mwa mabawa yako,
9. mbali na mashambulio ya waovu,mbali na maadui zangu hatari wanaonizunguka.
10. Hao hawana huruma yoyote moyoni;wamejaa maneno ya kujigamba.
11. Wananifuatia na kunizunguka;wananivizia waniangushe chini.
12. Wako tayari kunirarua kama simba:Kama mwanasimba aviziavyo mawindo.
13. Inuka, ee Mwenyezi-Mungu,uwakabili na kuwaporomosha.Kwa upanga uiokoe nafsi yangu kutoka kwa waovu.
14. Kwa mkono wako, ee Mwenyezi-Mungu,uniokoe mikononi mwa watu hao,watu ambao riziki yao ni dunia hii tu. Uwajaze adhabu uliyowawekea,wapate ya kuwatosha na watoto wao,wawaachie hata na wajukuu zao.