Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 17:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ee Mwenyezi-Mungu usikie kisa changu cha haki,usikilize kilio changu,uitegee sikio sala yangu isiyo na hila.

2. Haki yangu na ije kutoka kwako,kwani wewe wajua jambo lililo la haki.

3. Wewe wajua kabisa moyo wangu;umenijia usiku, kunichunguza,umenitia katika jaribio;hukuona uovu ndani yangu,sikutamka kitu kisichofaa.

4. Kuhusu matendo watendayo watu;mimi nimeitii amri yako,nimeepa njia ya wadhalimu.

Kusoma sura kamili Zaburi 17