4. Lakini wanaoabudu miungu mingine,watapata mateso mengi.Tambiko ya damu sitaitolea kamwe,na majina ya miungu hiyo sitayataja.
5. Wewe ee Mwenyezi-Mungu ndiwe riziki yangu kuu,majaliwa yangu yamo mikononi mwako.
6. Umenipimia sehemu nzuri sana;naam, urithi wangu ni wa kupendeza.
7. Namsifu Mwenyezi-Mungu kwa kuniongoza,usiku dhamiri yangu yanionya.
8. Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima;yuko pamoja nami, wala sitatikisika.
9. Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia,nami nitakaa salama salimini.
10. Naam wewe hutaiacha nafsi yangu kuzimu,hutaniacha mimi mwaminifu wako nipate kuoza.