Agano la Kale

Agano Jipya

Zaburi 11:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kwake Mwenyezi-Mungu nakimbilia usalama;mnawezaje basi kuniambia:“Ruka kama ndege, mpaka milimani,

2. maana waovu wanavuta pinde;wameweka mishale tayari juu ya uta,wawapige mshale watu wema gizani!

3. Kama misingi ikiharibiwa,mtu mwadilifu atafanya nini?”

4. Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;kiti cha enzi cha Mwenyezi-Mungu kiko mbinguni.Kwa macho yake huwachungulia wanadamu,na kujua kila kitu wanachofanya.

Kusoma sura kamili Zaburi 11