1. Kwake Mwenyezi-Mungu nakimbilia usalama;mnawezaje basi kuniambia:“Ruka kama ndege, mpaka milimani,
2. maana waovu wanavuta pinde;wameweka mishale tayari juu ya uta,wawapige mshale watu wema gizani!
3. Kama misingi ikiharibiwa,mtu mwadilifu atafanya nini?”
4. Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;kiti cha enzi cha Mwenyezi-Mungu kiko mbinguni.Kwa macho yake huwachungulia wanadamu,na kujua kila kitu wanachofanya.