Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 21:40-43 Biblia Habari Njema (BHN)

40. Miji yote waliyopewa wazawa wa Merari, yaani jamaa za Walawi zilizobaki, ilikuwa kumi na miwili.

41. Jumla ya miji yote ambayo Walawi walipewa katika maeneo ya Waisraeli ilikuwa arubaini na minane pamoja na mbuga zao za malisho.

42. Kila mmoja kati ya miji hii ulizungukwa na mbuga za malisho.

43. Basi, Mwenyezi-Mungu aliwapa Waisraeli nchi yote ambayo alikuwa amewaahidi wazee wao. Nao wakaimiliki na kuishi humo.

Kusoma sura kamili Yoshua 21