Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 20:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Yoshua,

2. awaambie Waisraeli hivi: “Jichagulieni miji ambamo mtu aweza kukimbilia usalama ambayo nilimwambia Mose akueleze.

3. Mtu yeyote akimuua mtu bila kukusudia anaweza kukimbilia katika mji mmojawapo na hivyo kumkwepa yule mtu aliye na jukumu la kulipiza kisasi cha damu.

4. Mwuaji atakimbilia katika mji mmojawapo na kusimama mlangoni mwa mji na kuwaeleza wazee wa mji huo kesi yake. Wazee watampokea ndani na kumpa mahali pa kuishi pamoja nao.

Kusoma sura kamili Yoshua 20