Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 19:16-31 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Hiyo ndiyo sehemu zilizopewa koo za kabila la Zebuluni miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

17. Kura ya nne ilizipata koo za kabila la Isakari.

18. Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,

19. Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,

20. Rabithi, Kishioni, Ebesi,

21. Remethi, En-ganimu, En-hada na Beth-pasesi.

22. Kadhalika, mpaka wao ulifika Tabori, Shahasuma, Beth-shemeshi na kuishia kwenye mto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.

23. Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Isakari; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

24. Kura ya tano ilizipata koo za kabila la Asheri.

25. Eneo la nchi yao lilikuwa na miji ya Helkathi, Hali, Beteni, Akshafi,

26. Alameleki, Amadi na Mishali. Kwa upande wa magharibi mpaka uligusana na Karmeli na Shihor-libnathi.

27. Kisha ukageuka kuelekea mashariki kwenda Beth-dagoni ambako unagusana na Zebuluni na bonde la Iftaheli. Halafu ukaendelea kaskazini hadi Beth-emeki, Neieli na kuzidi kuelekea kaskazini hadi Kabuli,

28. Ebroni, Rehobu, Hamoni, Kana hadi Sidoni Kuu.

29. Hapo, mpaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwamo ni Maharabu, Akzibu,

30. Uma, Afeka na Rehobu. Jumla ya miji waliyopewa ni ishirini na miwili pamoja na vijiji vyake.

31. Sehemu hizo ndizo zilizopewa koo za kabila la Asheri; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Kusoma sura kamili Yoshua 19