16. Hiyo ndiyo sehemu zilizopewa koo za kabila la Zebuluni miji hiyo pamoja na vijiji vyake.
17. Kura ya nne ilizipata koo za kabila la Isakari.
18. Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19. Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20. Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21. Remethi, En-ganimu, En-hada na Beth-pasesi.
22. Kadhalika, mpaka wao ulifika Tabori, Shahasuma, Beth-shemeshi na kuishia kwenye mto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.
23. Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Isakari; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.
24. Kura ya tano ilizipata koo za kabila la Asheri.