Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 19:15-25 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Ukajumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Yidala na Bethlehemu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

16. Hiyo ndiyo sehemu zilizopewa koo za kabila la Zebuluni miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

17. Kura ya nne ilizipata koo za kabila la Isakari.

18. Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,

19. Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,

20. Rabithi, Kishioni, Ebesi,

21. Remethi, En-ganimu, En-hada na Beth-pasesi.

22. Kadhalika, mpaka wao ulifika Tabori, Shahasuma, Beth-shemeshi na kuishia kwenye mto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.

23. Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Isakari; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

24. Kura ya tano ilizipata koo za kabila la Asheri.

25. Eneo la nchi yao lilikuwa na miji ya Helkathi, Hali, Beteni, Akshafi,

Kusoma sura kamili Yoshua 19