Agano la Kale

Agano Jipya

Yoshua 15:58-63 Biblia Habari Njema (BHN)

58. Vilevile miji ya Halhuli, Beth-suri, Gedori,

59. Maarathi, Beth-anothi na Eltekoni. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake.

60. Kadhalika walipewa Kiriath-baali, uitwao pia Kiriath-yearimu, na Raba. Jumla ya miji waliyopewa ni miwili pamoja na vijiji vyake.

61. Miji ya nyikani ilikuwa Beth-araba, Midini, Sekaka,

62. Nibshani, Mji wa Chumvi na Engedi. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake.

63. Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalemu, na mpaka leo Wayebusi bado wanaishi mjini humo pamoja na watu wa Yuda.

Kusoma sura kamili Yoshua 15