1. Neno la Mwenyezi-Mungu likamjia Yona mara ya pili:
2. “Nenda Ninewi, ule mji mkuu, ukawatangazie watu ujumbe niliokupa.”
3. Basi, Yona akaondoka, akaenda Ninewi kama Mwenyezi-Mungu alivyomwagiza.Mji wa Ninewi ulikuwa mkubwa sana. Upana wake ulikuwa mwendo wa siku tatu.
4. Alipowasili, Yona aliingia mjini, na baada ya kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: “Bado siku arubaini tu na mji huu wa Ninewi utaangamizwa!”