Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 9:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Yeye peke yake alizitandaza mbingu,na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

9. Ndiye aliyezifanya nyota angani:Dubu, Orioni, Kilimia, na nyota za kusini.

10. Ndiye atendaye makuu yasiyoeleweka,mambo ya ajabu yasiyo na idadi.

11. Loo! Hupita karibu nami nisimwone,kisha huenda zake bila ya mimi kumtambua.

12. Tazama! Yeye huchukua anachotaka;nani awezaye kumzuia?Nani awezaye kumwuliza: ‘Unafanya nini?’

13. “Mungu hatazuia hasira yake;chini yake wainama kwa hofu Rahabu na wasaidizi wake.

Kusoma sura kamili Yobu 9