Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 9:4-20 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Yeye ni mwenye hekima mno na nguvu nyingi,nani aliyepingana naye, akashinda?

5. Yeye huiondoa milima bila yenyewe kutambua,huibomolea mbali kwa hasira yake.

6. Yeye huitikisa dunia kutoka mahali pake,na nguzo zake zikatetemeka.

7. Huliamuru jua lisichomozehuziziba nyota zisiangaze.

8. Yeye peke yake alizitandaza mbingu,na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

9. Ndiye aliyezifanya nyota angani:Dubu, Orioni, Kilimia, na nyota za kusini.

10. Ndiye atendaye makuu yasiyoeleweka,mambo ya ajabu yasiyo na idadi.

11. Loo! Hupita karibu nami nisimwone,kisha huenda zake bila ya mimi kumtambua.

12. Tazama! Yeye huchukua anachotaka;nani awezaye kumzuia?Nani awezaye kumwuliza: ‘Unafanya nini?’

13. “Mungu hatazuia hasira yake;chini yake wainama kwa hofu Rahabu na wasaidizi wake.

14. Nitawezaje basi kumjibu Mungu?Nitachagua wapi maneno ya kumwambia?

15. Ingawa sina hatia, siwezi kumjibu.Lazima kumwomba anihurumie huyo mshtaki wangu.

16. Hata kama ningemwita naye akajibu,nisingeweza kuamini kuwa ananisikiliza.

17. Yeye huniponda kwa dhoruba;huongeza majeraha yangu bila sababu.

18. Haniachi hata nipumue;maisha yangu huyajaza uchungu.

19. Kama ni kushindana, yeye ana nguvu mno!Na kama ni kutafuta juu ya haki,nani atakayemleta mahakamani?

20. Ingawa sina hatia, maneno yangu yenyewe yangenihukumu;ingawa sina lawama, angenithibitisha kuwa mpotovu.

Kusoma sura kamili Yobu 9