Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 9:24-31 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Nchi ikitiwa watu waovu katika utawala wa mwovu,Mungu huyafumba macho ya mahakimu wake!Kama si yeye afanyaye hivyo, ni nani basi?

25. “Siku zangu zaenda mbio kuliko mpiga mbio;zinakimbia bila kuona faida.

26. Zapita kasi kama mashua ya matete;kama tai anayerukia mawindo yake.

27. Nasema: ‘Nitasahau lalamiko langu,niondoe uso wangu wa huzuni na kuwa na furaha!’

28. Lakini nayaogopa maumivu yangu yote,kwani najua Mungu hataniona kuwa sina hatia.

29. Ikiwa nitahukumiwa kuwa na hatia,ya nini basi nijisumbue bure?

30. Hata kama nikitawadha kwa theluji,na kujitakasa mikono kwa sabuni,

31. hata hivyo, atanitumbukiza shimoni kwenye uchafu,na mavazi yangu yataniona kuwa kinyaa.

Kusoma sura kamili Yobu 9