Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 9:12-15 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Tazama! Yeye huchukua anachotaka;nani awezaye kumzuia?Nani awezaye kumwuliza: ‘Unafanya nini?’

13. “Mungu hatazuia hasira yake;chini yake wainama kwa hofu Rahabu na wasaidizi wake.

14. Nitawezaje basi kumjibu Mungu?Nitachagua wapi maneno ya kumwambia?

15. Ingawa sina hatia, siwezi kumjibu.Lazima kumwomba anihurumie huyo mshtaki wangu.

Kusoma sura kamili Yobu 9