Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 8:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Tegemeo lao huvunjikavunjika,tumaini lao ni utando wa buibui.

15. Wanaegemea nyumba yao lakini haitasimama,huishikilia lakini haidumu.

16. Jua litokapo yeye hustawi;hueneza matawi yake bustanini mwake.

17. Mizizi yake hujisokotasokota kwenye mawenaye aenda kuchunguza ndani ya mwamba.

18. Lakini akiangamizwa kutoka makao yake,hayo yatamkana yakisema: ‘Sijapata kukuona.’

19. Tazama, huo ndio mwisho wa furaha ya mtu huyo,na mahali pao patachipua wengine.

20. “Tazama! Mungu hatamkataa mtu asiye na hatia,wala kuwasaidia waovu.

Kusoma sura kamili Yobu 8