Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 7:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. “Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu;jicho langu halitaona jema lolote tena.

8. Anayeniona sasa, hataniona tena,punde tu ukinitazama nitakuwa nimetoweka.

9. Kama wingu lififiavyo na kutowekandivyo nao watu washukavyo kuzimu bila kurudi.

10. Anayeondoka harudi tena kwa jamaa yake,na pale alipokuwa anaishi husahaulika mara.

11. “Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu kuongea;nitasema kwa msongo wa roho yangu,nitalalamika kwa uchungu wa nafsi yangu.

12. Je, mimi ni bahari au dude la baharinihata uniwekee mlinzi?

13. Nikisema, ‘Kitanda kitanipumzisha,malazi yangu yatanipunguzia malalamiko yangu,’

14. wewe waja kunitia hofu kwa ndoto,wanitisha kwa kuniletea maono;

Kusoma sura kamili Yobu 7