Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 7:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mwili wangu umejaa mabuu na uchafu;ngozi yangu imekauka na kutokwa na usaha wa jipu.

6. Siku zangu zapita kasi kuliko gurudumu la mshonaji,nazo zafikia mwisho wake bila matumaini.

7. “Kumbuka, maisha yangu ni pumzi tu;jicho langu halitaona jema lolote tena.

8. Anayeniona sasa, hataniona tena,punde tu ukinitazama nitakuwa nimetoweka.

9. Kama wingu lififiavyo na kutowekandivyo nao watu washukavyo kuzimu bila kurudi.

Kusoma sura kamili Yobu 7