Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 7:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Binadamu anayo magumu duniani,na siku zake ni kama siku za kibarua!

2. Yeye ni kama mtumwa atamaniye kivuli,kama mwajiriwa angojaye kwa hamu mshahara wake.

3. Basi nimepangiwa miezi na miezi ya ubatili,yangu ni majonzi usiku hata usiku.

4. Nilalapo nasema, ‘Nitaamka lini?’Kwani saa za usiku huwa ndefu sana;nagaagaa kitandani mpaka kuche!

5. Mwili wangu umejaa mabuu na uchafu;ngozi yangu imekauka na kutokwa na usaha wa jipu.

Kusoma sura kamili Yobu 7