Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 6:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Sina hamu ya kuvigusa vyakula hivyo,hivyo ni vyakula vyangu vichukizavyo.”

8. “Laiti ningejaliwa ombi langu,Mungu akanipatia kile ninachotamani:

9. Kwamba angekuwa radhi kunipondaponda,angenyosha mkono wake anikatilie mbali!

10. Hiyo ingekuwa faraja yangu,ningefurahi katika maumivu yasiyo na huruma.

11. Lakini sina nguvu ya kuweza kuendelea;sijui mwisho wangu utakuwaje, nipate kuvumilia.

Kusoma sura kamili Yobu 6