Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 6:24-30 Biblia Habari Njema (BHN)

24. “Nifundisheni, nami nitanyamaza.Nielewesheni jinsi nilivyokosea.

25. Maneno ya kweli yana nguvu kubwa!Lakini makaripio yenu yananikosoa nini?

26. Je, mnadhani kwamba mwaweza kuyakosoa maneno?Maneno ya mtu aliyekata tamaa ni upepo tu.

27. Nyinyi mnathubutu hata kuwapigia yatima kura;mnawapigia bei hata marafiki zenu!

28. Lakini sasa niangalieni tafadhali.Mimi sitasema uongo mbele yenu.

29. Acheni tafadhali, kusiwe na uovu;acheni sasa, kwani mimi ni mnyofu.

30. Je, mnadhani kwamba nimesema uovu?Je, mnafikiri mimi siyatambui machungu?

Kusoma sura kamili Yobu 6