Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 6:19-26 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Misafara ya Tema hutafuta tafuta,wasafiri wa Sheba hutumaini.

20. Huchukizwa kwa kutumaini bure,hufika kwenye vijito hivyo na kuudhika.

21. Nyinyi mmekuwa kama vijito hivyo,mwaona balaa yangu na kuogopa.

22. Je, nimesema mnipe zawadi?Au mnitolee rushwa kwa mali zenu?

23. Au mniokoe makuchani mwa adui?Au mnikomboe mkononi mwa wadhalimu?

24. “Nifundisheni, nami nitanyamaza.Nielewesheni jinsi nilivyokosea.

25. Maneno ya kweli yana nguvu kubwa!Lakini makaripio yenu yananikosoa nini?

26. Je, mnadhani kwamba mwaweza kuyakosoa maneno?Maneno ya mtu aliyekata tamaa ni upepo tu.

Kusoma sura kamili Yobu 6