Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 6:18-30 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Misafara hupotea njia wakitafuta maji,hupanda nyikani na kufia huko.

19. Misafara ya Tema hutafuta tafuta,wasafiri wa Sheba hutumaini.

20. Huchukizwa kwa kutumaini bure,hufika kwenye vijito hivyo na kuudhika.

21. Nyinyi mmekuwa kama vijito hivyo,mwaona balaa yangu na kuogopa.

22. Je, nimesema mnipe zawadi?Au mnitolee rushwa kwa mali zenu?

23. Au mniokoe makuchani mwa adui?Au mnikomboe mkononi mwa wadhalimu?

24. “Nifundisheni, nami nitanyamaza.Nielewesheni jinsi nilivyokosea.

25. Maneno ya kweli yana nguvu kubwa!Lakini makaripio yenu yananikosoa nini?

26. Je, mnadhani kwamba mwaweza kuyakosoa maneno?Maneno ya mtu aliyekata tamaa ni upepo tu.

27. Nyinyi mnathubutu hata kuwapigia yatima kura;mnawapigia bei hata marafiki zenu!

28. Lakini sasa niangalieni tafadhali.Mimi sitasema uongo mbele yenu.

29. Acheni tafadhali, kusiwe na uovu;acheni sasa, kwani mimi ni mnyofu.

30. Je, mnadhani kwamba nimesema uovu?Je, mnafikiri mimi siyatambui machungu?

Kusoma sura kamili Yobu 6