Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 40:4-15 Biblia Habari Njema (BHN)

4. “Mimi sifai kitu nitakujibu nini?Naufunga mdomo wangu.

5. Nilithubutu kusema na sitasema tena.Nilisisitiza lakini sitaendelea kusema zaidi.”

6. Hapo Mwenyezi-Mungu akamjibu kutoka kimbunga:

7. “Jikaze kama mwanamume.Nitakuuliza, nawe utanijibu.

8. Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?

9. Je, una nguvu kama mimi Mungu?Waweza kunguruma kwa sauti kama yangu?

10. “Basi, jioneshe kuwa na fahari na ukuu,ujipambe kwa utukufu na fahari.

11. Wamwagie watu hasira yako kuu;mwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.

12. Mwangalie kila mwenye kiburi na kumporomosha,uwakanyage waovu mahali walipo.

13. Wazike wote pamoja ardhini;mfunge kila mmoja kwa kifungo cha kifo.

14. Hapo nitakutambua,kwamba nguvu yako mwenyewe imekupa ushindi.

15. “Liangalie lile dude Behemothi,nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.Hilo hula nyasi kama ng'ombe,

Kusoma sura kamili Yobu 40