Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 40:27-32 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Je, wadhani litakusihi uliachilie?Je, litazungumza nawe kwa upole?

28. Je, litafanya mapatano nawe,ulichukue kuwa mtumishi wako milele?

29. Je, utacheza nalo kama ndege,au kulifunga kamba licheze na wajakazi wako?

30. Wadhani wavuvi watashindania bei yake?Je, wafanyabiashara watathubutu kulikata na kugawana?

31. Je, waweza kuichoma ngozi yake kwa mikuki,au kichwa chake kwa mfumo wa kuvua samaki?

32. Jaribu tu kuligusa, uone cha mtema kuni;Kamwe hutarudia tena kufanya hivyo!

Kusoma sura kamili Yobu 40