Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 40:15-24 Biblia Habari Njema (BHN)

15. “Liangalie lile dude Behemothi,nililoliumba kama nilivyokuumba wewe.Hilo hula nyasi kama ng'ombe,

16. lakini mwilini lina nguvu ajabu,na misuli ya tumbo lake ni imara.

17. Huufanya mkia wake mgumu kama mwerezi,mishipa ya mapaja yake imeshonwa pamoja.

18. Mifupa yake ni mabomba ya shaba,viungo vyake ni kama pao za chuma.

19. “Hilo ni la kwanza la ajabu kati ya viumbe vyangu!Ni mimi Muumba wake niwezaye kulishinda.

20. Milima wanamocheza wanyama wote wa porinihutoa chakula chake.

21. Hujilaza chini ya vichaka vya miiba,na kujificha kati ya matete mabwawani.

22. Hujisitiri katika vivuli vya vichaka vya miibana vya miti iotayo kando ya vijito.

23. Mto ukifurika haliogopi,halitishiki hata mto Yordani ukilifurikia kinywani.

24. Nani awezaye kuliziba macho na kuliteka?Nani awezaye kulitoboa pua kwa mtego?

Kusoma sura kamili Yobu 40