Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 40:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu akaendelea kumwambia Yobu:

2. “Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu?Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”

3. Kisha Yobu akamjibu Mwenyezi-Mungu:

4. “Mimi sifai kitu nitakujibu nini?Naufunga mdomo wangu.

5. Nilithubutu kusema na sitasema tena.Nilisisitiza lakini sitaendelea kusema zaidi.”

6. Hapo Mwenyezi-Mungu akamjibu kutoka kimbunga:

7. “Jikaze kama mwanamume.Nitakuuliza, nawe utanijibu.

8. Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?

Kusoma sura kamili Yobu 40