1. Mwenyezi-Mungu akaendelea kumwambia Yobu:
2. “Je, wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Nguvu?Wewe unayebishana nami Mungu, basi jibu mambo hayo!”
3. Kisha Yobu akamjibu Mwenyezi-Mungu:
4. “Mimi sifai kitu nitakujibu nini?Naufunga mdomo wangu.
5. Nilithubutu kusema na sitasema tena.Nilisisitiza lakini sitaendelea kusema zaidi.”
6. Hapo Mwenyezi-Mungu akamjibu kutoka kimbunga:
7. “Jikaze kama mwanamume.Nitakuuliza, nawe utanijibu.
8. Je, unataka kweli kubatilisha hukumu yangu,kuniona nina hatia ili wewe usiwe na hatia?