Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 39:19-23 Biblia Habari Njema (BHN)

19. “Je, Yobu, ndiwe uliyewapa farasi nguvu,ukawavika shingoni manyoya marefu?

20. Je, ni wewe unayemfanya farasi aruke kama nzige?Mlio wake wa maringo ni wa ajabu!

21. Huparapara ardhi mabondeni kwa pupa;hukimbilia kwenye mapigano kwa nguvu zake zote.

22. Farasi huicheka hofu, na hatishiki;wala upanga hauwezi kumrudisha nyuma.

23. Silaha wachukuazo wapandafarasi,hugongana kwa sauti na kungaa juani.

Kusoma sura kamili Yobu 39