Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 39:18-27 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Lakini akianza kukimbia,humcheka hata farasi na mpandafarasi.

19. “Je, Yobu, ndiwe uliyewapa farasi nguvu,ukawavika shingoni manyoya marefu?

20. Je, ni wewe unayemfanya farasi aruke kama nzige?Mlio wake wa maringo ni wa ajabu!

21. Huparapara ardhi mabondeni kwa pupa;hukimbilia kwenye mapigano kwa nguvu zake zote.

22. Farasi huicheka hofu, na hatishiki;wala upanga hauwezi kumrudisha nyuma.

23. Silaha wachukuazo wapandafarasi,hugongana kwa sauti na kungaa juani.

24. Farasi husonga mbele, akitetemeka kwa hasira;tarumbeta iliapo, yeye hasimami.

25. Kila ipigwapo tarumbeta, yeye hutoa sauti;huisikia harufu ya vita toka mbali,huusikia mshindo wa makamandawakitoa amri kwa makelele.

26. “Je, mwewe amejifunza kwako jinsi ya kuruka,na kunyosha mabawa yake kuelekea kusini?

27. Je, tai hupaa juu kwa amri yako,na kuweka kiota chake juu milimani?

Kusoma sura kamili Yobu 39