20. Je, nani anathubutu kumwambia: Nataka kuongea?Nani aseme apate balaa?
21. “Ghafla mtu hawezi tena kuona waziwazi:Jua limefichika nyuma ya mawingu,na upepo umefagia anga!
22. Mngao mzuri hutokea kaskazini;Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.
23. Mungu Mwenye Nguvu asiyeweza kufikiwa na mtu,uwezo na uadilifu wake ni mkuu,amejaa wema wala hapotoshi haki kamwe.
24. Kwa hiyo, watu wote humwogopa;yeye hamjali mtu yeyote mwenye kiburi.”