Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 37:17-24 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Wewe wajiona umevaa nguo za joto sana,wakati upepo wa kusi unaivamia nchi.

18. Je, waweza, kuzitandaza mbingu kama yeyezikawa ngumu kama kioo cha shaba?

19. Tufundishe tutakachomwambia Mungu;maana hoja zetu si wazi, tumo gizani.

20. Je, nani anathubutu kumwambia: Nataka kuongea?Nani aseme apate balaa?

21. “Ghafla mtu hawezi tena kuona waziwazi:Jua limefichika nyuma ya mawingu,na upepo umefagia anga!

22. Mngao mzuri hutokea kaskazini;Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.

23. Mungu Mwenye Nguvu asiyeweza kufikiwa na mtu,uwezo na uadilifu wake ni mkuu,amejaa wema wala hapotoshi haki kamwe.

24. Kwa hiyo, watu wote humwogopa;yeye hamjali mtu yeyote mwenye kiburi.”

Kusoma sura kamili Yobu 37