Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 37:13-23 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Mungu hutekeleza matakwa yake duniani;iwe ni kwa ajili ya kuwaadhibu watu,au kwa ajili ya kuonesha upendo wake.

14. “Unapaswa kusikiliza Yobu;nyamaza, usikilize maajabu ya Mungu.

15. Je, wajua jinsi Mungu anavyovipa amri yake,na kufanya umeme wa mawingu yake ungae?

16. Je, wajua jinsi mawingu yanavyoelea angani?Ndizo kazi za ajabu za yule aliye mkamilifu wa maarifa!

17. Wewe wajiona umevaa nguo za joto sana,wakati upepo wa kusi unaivamia nchi.

18. Je, waweza, kuzitandaza mbingu kama yeyezikawa ngumu kama kioo cha shaba?

19. Tufundishe tutakachomwambia Mungu;maana hoja zetu si wazi, tumo gizani.

20. Je, nani anathubutu kumwambia: Nataka kuongea?Nani aseme apate balaa?

21. “Ghafla mtu hawezi tena kuona waziwazi:Jua limefichika nyuma ya mawingu,na upepo umefagia anga!

22. Mngao mzuri hutokea kaskazini;Mungu amezungukwa na utukufu wa kutisha.

23. Mungu Mwenye Nguvu asiyeweza kufikiwa na mtu,uwezo na uadilifu wake ni mkuu,amejaa wema wala hapotoshi haki kamwe.

Kusoma sura kamili Yobu 37