Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 36:9-20 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Mungu huwaonesha matendo yao maovu,na kwamba wao ni watu wenye kiburi.

10. Huwafungua masikio wasikie mafunzo,na kuwaamuru warudi na kuacha uovu.

11. Wakimtii Mungu na kumtumikia,hufanikiwa katika siku zao zote;miaka yao yote huwa ya furaha.

12. Lakini wasipomtii, huangamia kwa upanga,na kufa kwa kukosa akili.

13. “Wasiomcha Mungu hupenda kukasirika,hawamlilii msaada anapowabana.

14. Hufa wangali bado vijana,maisha yao huisha kama ya walawiti.

15. Lakini Mungu huwaokoa wanyonge kwa unyonge waohutumia shida zao kuwafumbua macho.

16. Mungu alikuvuta akakutoa taabuni,akakuweka mahali pa wasaa pasipo shida,na mezani pako akakuandalia vinono.

17. “Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu,hukumu ya haki imekukumba.

18. Jihadhari ghadhabu isije ikakufanya ukadhihaki,au ukubwa wa mali za kukukomboa ukakupotosha.

19. Je, kilio chako kitafaa kukutoa taabuni,au nguvu zako zote zitakusaidia?

20. Usitamani usiku uje,ambapo watu hufanywa watoweke walipo.

Kusoma sura kamili Yobu 36