Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 36:12-31 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Lakini wasipomtii, huangamia kwa upanga,na kufa kwa kukosa akili.

13. “Wasiomcha Mungu hupenda kukasirika,hawamlilii msaada anapowabana.

14. Hufa wangali bado vijana,maisha yao huisha kama ya walawiti.

15. Lakini Mungu huwaokoa wanyonge kwa unyonge waohutumia shida zao kuwafumbua macho.

16. Mungu alikuvuta akakutoa taabuni,akakuweka mahali pa wasaa pasipo shida,na mezani pako akakuandalia vinono.

17. “Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu,hukumu ya haki imekukumba.

18. Jihadhari ghadhabu isije ikakufanya ukadhihaki,au ukubwa wa mali za kukukomboa ukakupotosha.

19. Je, kilio chako kitafaa kukutoa taabuni,au nguvu zako zote zitakusaidia?

20. Usitamani usiku uje,ambapo watu hufanywa watoweke walipo.

21. Jihadhari! Usiuelekee uovumaana umepatiwa mateso kukuepusha na uovu.

22. Kumbuka ukuu wa uwezo wa Mungu;nani awezaye kumfundisha kitu?

23. Nani basi aliyeweza kumpangia njia yake,au awezaye kumwambia: ‘Umekosea?’

24. “Usisahau kuyasifu matendo yake;ambayo watu wameyashangilia.

25. Watu wote wameona aliyofanya Mungu;binadamu huyaona kutoka mbali.

26. Mungu ni mkuu mno hata hatuwezi kumjua;muda wa maisha yake hauchunguziki.

27. Yeye huyavuta kwake maji ya bahari,na kutoka ukungu hufanya matone ya mvua.

28. Huyafanya mawingu yanyeshe mvua,na kuwatiririshia binadamu kwa wingi.

29. Nani ajuaye jinsi mawingu yatandavyo,au jinsi radi ingurumavyo angani kwake?

30. Yeye huutandaza umeme wake kumzunguka,na kuvifunika vilindi vya bahari.

31. Kwa mvua huwalisha watuna kuwapatia chakula kwa wingi.

Kusoma sura kamili Yobu 36