4. Basi, na tuchague lililo sawa,tuamue miongoni mwetu lililo jema.
5. Basi, Yobu ametamka: ‘Mimi Yobu sina hatia,Mungu ameniondolea haki yangu.
6. Ingawa sina hatia naonekana kuwa mwongo;kidonda changu hakiponyeki ingawa sina kosa.’
7. Ni nani aliye kama Yobuambaye kwake ubaradhuli ni kama kunywa maji?
8. Huandamana na watenda maovuhutembea na watu waovu.
9. Maana amesema, ‘Mtu hapati faida yoyote,kujisumbua kumpendeza Mungu.’
10. “Kwa hiyo nisikilizeni, enyi wenye ujuzi.Mungu kamwe hawezi kufanya uovu;Mungu Mwenye Nguvu hawezi kufanya kosa.